Psalms 10:2-7
2 aKatika kiburi chake, mwovu humtesa maskini,
waovu na wanaswe katika hila wanazozitunga.
3 Hujivunia tamaa za moyo wake;
humbariki mlafi na kumtukana Bwana.
4 bKatika kiburi chake, mwovu hamtafuti Mungu,
katika mawazo yake yote
hakuna nafasi ya Mungu.
5 cNjia zake daima hufanikiwa;
hujivuna na amri zako ziko mbali naye,
huwacheka kwa dharau adui zake wote.
6 dAnajisemea mwenyewe, “Hakuna kitakachonitikisa,
daima nitakuwa na furaha,
kamwe sitakuwa na shida.”
7 eKinywa chake kimejaa laana, uongo na vitisho;
shida na ubaya viko chini ya ulimi wake.
Copyright information for
SwhKC